Showing posts with label Kwa wale wanathamini kazi niitendayo. Show all posts

Kwa wale wanathamini kazi niitendayo naomba SHARE ujumbe huu

No comments
Kwa wale wanathamini kazi niitendayo naomba SHARE ujumbe huu
Kama sehemu ya ushiriki na mchango wangu katika Mchakato wa Katiba Mpya ni kuuelimisha umma wa watanzania juu ya mchakato wa kupata Katiba Mpya kwa kuandika Makala Maalum za kiuchambuzi kuhusu mchakato na maudhui ya mchakato.
Kila wiki ninaandikia Gazeti ya RAI kila Alhamis na Gazeti la Mwananchi kila Jumapili.
Kazi ninayoifanya ni ya kujitolea na ni kwa mapenzi yangu mema na kama mchango wangu mdogo ili sisi sote kama Taifa tufikie lengo letu la pamoja la kupata Katiba Mpya. Kazi hii sio rahisi hata kidogo, ni ngumu na ninaifanya kiubishi ubishi nikiamini watanzania wenzangu wana haki ya kujua taarifa za mchakato kutoka pande zote za shilingi.
Kwa kazi hii sihitaji malipo ya aina yoyote isipokuwa moja tu, kwamba haijalishi msimamo wowote ulio nao katika mchakato lakini nitendee haki kwa kusoma maudhui ya mchakato wa Katiba Mpya, ambayo ni pamoja na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sheria ya Kura ya Maoni, Katiba ya 1977, Rasimu ya Katiba Toleo la Pili, Katiba Inayopendekezwa na ukipata muda nitashukuru na nitapata faraja kama ukisoma maandiko niandikayo.
Naomba ieleweke, simlazimishi mtu kusoma niandikacho bali kwa heshima kubwa ninawakaribisha kusoma maandiko yangu, napenda kukosolewa kwa hoja, kwa sababu, napenda tujadiliane, napenda sote tuujue ukweli. Imani yangu ni kwamba sote tukishiriki, tukijadiliana, tukiulizana maswali yasiyo mepesi na tukipeana majibu yasiyo mepesi.
Kwa wale mnaothamini mchango wangu mdogo naomba Muusambaze Ujumbe huu kwa ku-SHARE na watu wengi zaidi pamoja na Makala yangu ya Gazeti la Mwananchi Jumapili iliyopita ambayo nimeiambatisha hapa.